Wednesday, January 24, 2018

TAFAKARI YA UHUSIANO WA HALI YA MAISHA YA GIDEONI NA MADHABAHU ALIYOKUWA AKIITUMIKIA BABA YAKE BAALI

Kutafakari uhusiano wa hali ya maisha ya Gideoni na madhabahu aliyokuwa akiitumikia baba yake ya Baali.

Waamuzi 6:11-32. Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. 12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. 13 Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani. 14 Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani.

Thursday, August 24, 2017

NAMNA YA KUMTWIKA BWANA FEDHEHA ULIYO NAYO



Na Mosses Benedict
Mawasiliano +255 762 371 383

 

MAELEKEZO; Somo hili tutatembea nalo taratibu kwa kadri ya neema ya Mungu na mfululizo nilionao        ndani ya moyo wangu. Yesu ni halisi na anasema Nenoi halisi ivo na hili somo hili halisi kabisa. Fuatilia somohili kila wiki kwa mfululizo tutakao kuwa nao kwa kadri ya majibu ya Mungu kwa watu wake hasa waliolemewa katikam kuishi. Omba kila usomapo hatua na msihi Mungu azidi kukufundusha katika Roho mtakatifu.
MATHAYO 11:28-30, Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na                     mzigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa  mimi           ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi

Tuesday, May 30, 2017

NAMNA AMBAVYO MUNGU ANAWEZA KUJIBU TUNAPOFANYA MAOMBI YA TOBA KATIKA MISINGI

Na Mosses Benedicto 
 Mawasiliano +255 762 371 383
Tunapofanya maombi ya toba katika misingi kwa kuachilia na kunyunyizia au kumwaga damu ya Yesu, kumbuka jambo hili muhimu, kuwa tunakuwa tunaachilia Roho ya Mungu itendayo kazi iliyo ndani ya damu ya mwana wake, kwa hiyo Roho wa Mungu anashuka na kuanza kufanya kazi (operation) katika eneo lolote ambalo mwana wa ufalme ameachiwa.

Roho hiyo inatenda kazi kwa namna au njia tofauti tofauti ambazo tunaweza kusema ni namna ya Mungu aliyehai kutenda kazi yake katika Roho yake, hivyo zifuatazo ni baadhi ya njia au namna ambavyo Mungu aliyehai anajibu ikiwa watu wake wameomba toba katika misingi au wamemkaribisha. Mungu anaweza kujibu au kujidhiirisha kwa namna tofauti tofauti unapomkaribisha juu ya misingi, baadhi ni izi zifuatazo;

Wednesday, May 24, 2017

UWEZA NA NGUVU ILIYOMO NDANI YA DAMU YA YESU JUU YA MISINGI NA INAVYOGUSA HALI YA MAISHA YA WATU YA BAADAE

Na Mosses Benedict
Mawasiliano +255 762 371 383


Haleluya mtu wa Mungu aliyehai, tumekuwa tukijifunza somo linalohusu masuala ya misingi angalau kwa kuingia ndani kidogo kidogo kadiri ya neema ya Mungu, karibu sasa tuendelee na nguvu iliyoko ndani ya damu ya Yesu, vitu inavyofanya katika misingi ikiwa wewe mwombaji umeomba maombi ya toba katika misingi
kuwa nami..............

Tunapozungumzia damu, hatuizungumzii tu damu kama kimiminika tunavyojua, ila kwa jicho la ndani au la kiroho tunazungumzia uhai uliomo ndani ya damu, siyo tu damu ila uhai uliomo ndani ya damu. Uhai ni roho inayoishi, inayotenda kazi. Tunapozungumzia damu ya Yesu tunazungumzia uhai au roho ya Mungu iliyomo ndani ya damu yake, hivyo tunapoachilia, nyunyizia au tunapomwaga damu ya Yesu katika eneo lolote, mfano juu ya ardhi, madhabahu, malango au vifungo, katika ulimwengu wa roho tunakuwa tunaachilia uhai au Roho itendayo kazi iliyomo ndani ya damu ya Yesu aliyehai ili itende kazi ambayo tunakuwa tukitamka wakati wa kuomba.

Wednesday, May 17, 2017

Mwendelezo wa mambo ya kufahamu yanayohusiana na misingi

03.03.  Malengo ya msingi

Kusudi la kujenga msingi mbele yako ni nini? wanaweka nini wanapoujenga msingi leo kwa ajili ya maisha yako ya baadae? Sababu za kusimamisha msingi mbele yako zipo kadhaa kama:
Kukuzungushia wigo ili ukitaka kuvuka ukutane na ukuta (mipaka ili usivuke) yaani vizuizi, vikwazo katika eneo fulani ili uzungukie humo humo kimaisha na kihuduma. Lengo la kukuwekea ukuta mbele, wigo au uzio ni usione mbele, uone giza tu, ukate tamaa, urudi nyuma, ujione huwezi, hufai, huna maana. Ukuta; ni kuziba mahali unapotakiwa upaone ili usipaone au unapotakiwa kwenda au kuvuka ili usivuke. Lengo ni uishi au ukae ndani ya eneo hilo hilo au mfumo huo huo ili uendelee kuona yale yale kama kuonewa, kudharauliwa ugumu n.k.

Wednesday, May 10, 2017

VITU MUHIMU VYA KUJUA KATIKA MASUALA YA MISINGI

Haleluya mtu wa Mungu, karibu katika mwendelezo wa masomo yetu. Kuna masuala au vitu vya kufahamu unapotaka kufanya maombi ya toba katika misingi ambavyo angalau vitaweka msukumo ndani yako wa kukusukuma kufanya maombi ya toba katika misingi, na leo tukaone kwa sehemu na tutaendelea tena siku nyingine. Bwana Yesu asifiwe

03. 01. Uhalali wa misingi

Misingi inaweza kuwa halali au ya uonevu; Biblia inasema tulikuwepo kabla ya kuumbwa kwa misingi ya dunia hii hivyo Mungu alipotaka kuleta ufalme wake hapa duniani, au alipoamua kutanua na kupanua ufalme wake wa mbinguni ili kuudhihirisha kwa namna ya kimwili alitengeneza mazingira kwanza (yaani eneo la kufikia msingi) ambayo ufalme wake utafikia na utaanzia kama mwanzo wa maisha au kama msingi wa ufalme wake na maisha ya watu wake. Mwanzo wa kuanzia ambako kulikuwa na utukufu wake, Uungu, uweza, umiliki na utawala wake au uzima katika yote ili uwe mwendelezo wa maisha ya baadae tokea katika msingi huo. Lakini dhambi iliingia katika msingi huo (Edeni) na kuanza kuachilia na kuzaa vitu tofauti (mauti) na vilivyokusudiwa tangu mwanzo (uzima) Warumi 5:12, Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi;

Saturday, May 6, 2017

Umuhimu au Malengo ya meza ya Bwana


By. Mwl MOSSES BENEDICTO 0762371383
Ni nini umuhimu wa meza ya Bwana? ni kwanini tushiriki meza ya Bwana? nini faida ya meza ya Bwana? Kuwa na nami katika somo hili/.............

     
       01.   Kumwingiza kila mshiriki katika agano.
Ukisoma baadhi ya maandiko katika biblia utaona hili jambo au jukumu ambalo linafanywa na makuhani waliopewa dhamana au mamlaka ya kuwaingiza washiriki katika agano kwa njia ya meza ya Bwana haijalishi washiriki wanajua kuwa kuishiriki meza ya Bwana kunawaingiza katika agano au hawajui, wanapenda kwa mioyo yao au hawapendi.