Thursday, August 24, 2017

NAMNA YA KUMTWIKA BWANA FEDHEHA ULIYO NAYO



Na Mosses Benedict
Mawasiliano +255 762 371 383

 

MAELEKEZO; Somo hili tutatembea nalo taratibu kwa kadri ya neema ya Mungu na mfululizo nilionao        ndani ya moyo wangu. Yesu ni halisi na anasema Nenoi halisi ivo na hili somo hili halisi kabisa. Fuatilia somohili kila wiki kwa mfululizo tutakao kuwa nao kwa kadri ya majibu ya Mungu kwa watu wake hasa waliolemewa katikam kuishi. Omba kila usomapo hatua na msihi Mungu azidi kukufundusha katika Roho mtakatifu.
MATHAYO 11:28-30, Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na                     mzigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa  mimi           ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi
Lengo kuu la somo hili ni; kuongeza kiwango cha uhuru ndani ya moyo wako kwa kuona Yesu akikutua mizigo unayopitia katika hali ya maisha yako, pamoja na ;
1.      Kujua kuwa kuna matatizo, shida, fedhea, aibu, taabu na au misiba iliyo ndani ya uwezo wako na iliyo nje na uwezo wako, na licha ya kuwa na watu wa kukuombea na kukushauri lakini ni mmoja tu wa kukusaidia katika yote ni mmoja tu yaani Yesu.
2.      kujua kuwa unaweza kufikia katika maisha yako na ukamwambia Mungu niue kama Eliya na hakuui, nitoe mahali hapa au nitoe katika kanisa hili, eneo, ofisi na hakutoi ila anaondoa tatizo lililokufikisha katika hali uliyomo na anakuacha hapohapo katika eneo lako, familia na au  ukoo kama ulivyokuwa. Maana yake anaondoa kinachokutesa, kinachokuumiza, kinachokupa shida, aibu, fedhea lakini wewe hakuondoi.
3.      Kujua kuwa kuna vyanzo mbalimbali vya kukupelekea kuingia katika hali ya majuto, vilio, kuugua nafsini mwako, magonjwa, kutozaa, kutoolewa au kutooa, kutofanikiwa lakini suluhisho la maisha yako ni ufunguo mmoja tu.
4.      Somo hili linalenga kukufundisha kuwa kuna kutazama shida uliyonayo kwa kujilinganisha na kanisa lako, kikundi au chama chako, mazingira, familia au ukoo, kaya na jamii, kundi rika na bado vipimo vya namna hii havizai utatuzi wa shida yako. Kwaiyo tazama kila tatizo kwa jicho la Yesu ndo utapata utatuzi kwa ajili ya maisha yako.
5.      Pia ndani ya somo hili andaa akili, ufahamu na fikra zako ili kujifunza namna ya kutua mzigo ili naye akusaidie kukutua mzigo, kwaiyo ujiandae kuwajibika wewe binafsi kumwendea Yesu maana yake onesha hali ya kuhitaji msaada kuwa wewe peke yako hauwezi.
Kwaiyo somo hili linakulenga wewe ndugu katika Kristo ambaye umefikia mahali au katika hali fulani kimaisha labda katika; ofisi unayofanyia kazi, mahangaiko ya uchumi, uhusiano na ndugu, mwenza au rafiki, huduma na utumishi, ugonjwa wa mda mrefu, pito fulani linalokuhumiza kila siku, linakusumbua  hadi umefika hatua kila ukilala unaona tatizo hilohilo kiasi cha kukosa furaha ya kuishi, umechoka, umehaibika, unajionea aibu, fedhea, hufai, umejikana, umefika hatua ukajitamkia vibaya lakini sikia
Neno la Bwana, katika hali hiyo ya kulemewa Yesu anakwambia ivi njoo nikutue mzigo. Umesikia Bwana Yesu anavyokwambia, nakuuliza umesikia? Soma hili andiko ukaone. Mathayo 11:28-30Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu; kwa maana nira yangu ni laini, na mzigo wangu ni mwepesi.
Bwana Yesu asifiwe mtu wa Mungu! Haleluya haleluya.
Naomba turudi katika kichwa cha somo letu cha namna ya kumtwika Yesu fedhea uliyonayo, na tuanze kuangalia kadri ya neema ya Mungu aliyehai katika Kristo Yesu;
Fedheha; ni hali ya aibu inayompata mtu kwasababu ya aidha tukio lililompata, hali anayopitia au matendo aliyoyafanya au aliyofanyiwa lakini kwa ujumla yeye binafsi anajishuhudia au anajionea aibu kwake binafsi, familia na kwa mwana jamii anayemzunguka.
Katika hali ya namna hii unaweza ukajiona au ukajihisi katika mazingira na hali ya namna tofautitofauti saana, ukawaza saana, ukapoteza mwelekeo wa maisha au tumaini. Ukajiona au ukajipangia vibaya, ukaona giza tupu mbele yako, ukaona hufai hata katika lolote kwa jinsi ya kibinadamu tena ukafikia hatua ya kujificha kwa marafiki zako, ndugu na jamii inayokuzunguka kwasababu ukitazama msiba ulionao, ugonjwa wako, taabu na shida ulizonazo, au hali uliyonayo vinakuzalia aibu, huzuni, majuto, masikitiko, fedhea, kujilaumu kwamba kwanini mimi ndani ya moyo na nafsini mwako.
Na Yesu anapokujia wewe uliyelemewa anataka aondoe yote hayo ndani ya nafsi yako na akupe raha nafsini mwako, amani, furaha, utulivu na uone hali mpya katika hali ya maisha yako maana ndiyo anavyokwambia kuwa atakupa raha nafsini mwako katika Mathayo 11:29,  Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu
Bwana yesu asifiwe! Bwana wetu Yesu Kristo asifiwe.
Kwaiyo kulingana na maandiko tunayotembea nayo, weka akili mwako hili jambo muhimum kuwa kuna watu wana mizigo, aibu, fedhea lakini bado haijawatesa kwa kiwango cha kuwalemea na ivo Yesu hajawatua mizigo yao, aibu na fedhea zao kwasbabu vitu walivyonavyo aidha ni vya kawaida, au wamepungukiwa tu na nguvu za kuwasaidia kubeba walivyonavyo ila mizigo hiyo iko ndani ya uwezo wao kabisa, au wamebeba vibaya, au wanataka kutua tu bila sababu na ivo Yesu anasema subiri kidogo kwanza mpaka ulemewe ndo uje kwangu nikutue mzigo wako.
Unaweza ukasema niue kama Eliya, lakini ujue Eliya hakusema niue kwasababu rahisi rahisi tu ni baada ya kuona hali na mazingira yote yamekuwa magumu kiasi ambacho hatamani tena kuishi na kama vile yamefika mwisho, unaweza ukamwambia nitoe katika njia hii au nitoe katika hali hii maana nimechoka na nimelemewa kama Yesu wakati wa kuelekea msalabani lakini hakuoi bali aidha anakutia nguvu za kukusaidia kutembea au anaondoa unachokiona ni tatizo kwako lakini wewe anakakuacha hapohapo. Haleluya! haleluya mtu wa Mungu aliyehai
Karibu katika somo hili, tuombeane kwa Mungu atupaye neema ili tuendelee nalo kwa kadri ya neema yake. Maombi yako juu ya huduma hii na madhabahu hii ni muhimu mbele za Bwana. 
Pia hii ni mara ya kwanza kwa somo hili na tutaendelea nalo kila wiki kwa mfululizo nilionao ndani yangu. 
 Mungu atupe neema, karibu katika Kristo Yesu.


No comments:

Post a Comment