Wednesday, January 24, 2018

TAFAKARI YA UHUSIANO WA HALI YA MAISHA YA GIDEONI NA MADHABAHU ALIYOKUWA AKIITUMIKIA BABA YAKE BAALI

Kutafakari uhusiano wa hali ya maisha ya Gideoni na madhabahu aliyokuwa akiitumikia baba yake ya Baali.

Waamuzi 6:11-32. Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. 12 Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. 13 Gideoni akamwambia, Ee Bwana wangu, ikiwa Bwana yu pamoja nasi, mbona mambo haya yote yametupata? Yako wapi matendo yake ya ajabu, waliyotuhadithia baba zetu, wakisema, Je! Siye Bwana, aliyetuleta huku kutoka Misri? Ila sasa ametutupa, naye ametutia katika mikono ya Midiani. 14 Bwana akamtazama, akasema, Enenda kwa uwezo wako huu, ukawaokoe Israeli na mkono wa Midiani.
Je! Si mimi ninayekutuma? 15 Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu. 16 Bwana akamwambia, Hakika nitakuwa pamoja nawe, nawe utawapiga Wamidiani kama mtu mmoja. 17 Naye akamwambia, Kama nimepata kibali mbele za macho yako, basi unionyeshe ishara, ya kuwa ndiwe wewe unayesema nami. 18 Tafadhali, usiondoke hapa hata nikujie, nikatoe zawadi yangu, na kuiweka mbele zako. Akasema, Nitangoja hata utakaporudi. 19 Basi Gideoni akaingia ndani, akaandaa mwana-mbuzi, na mikate isiyotiwa chachu, ya efa ya unga; akaitia ile nyama katika kikapu, akautia mchuzi katika nyungu, akamletea hapo nje chini ya mwaloni, akampa. 20 Naye malaika wa Mungu akamwambia, Itwae nyama na mikate isiyotiwa chachu, uiweke juu ya mwamba huu, ukaumwage huu mchuzi.

Akafanya hivyo. 21 Ndipo malaika wa Bwana akanyosha ncha ya fimbo ile iliyokuwa mkononi mwake, akaigusa ile nyama na ile mikate; moto ukatoka mwambani, ukaiteketeza ile nyama na mikate; malaika wa Bwana akaondoka mbele ya macho yake. 22 Gideoni akaona ya kuwa ni malaika wa Bwana; Gideoni akasema, Ole wangu, Ee Bwana MUNGU! Kwa kuwa nimemwona Bwana uso kwa uso. 23 Bwana akamwambia Amani iwe pamoja nawe; usiogope; hutakufa. 24 Ndipo Gideoni akamjengea Bwana madhabahu hapo, akaiita jina lake, Yehova-Shalomu; hata hivi leo iko huko katika Ofra ya Waabiezeri. 25 Ikawa usiku uo huo Bwana akamwambia, Mtwae ng'ombe wa baba yako, yaani ng'ombe wa pili, wa miaka saba, ukaiangushe madhabahu ya Baali, aliyo nayo baba yako, ukaikate Ashera ile iliyo karibu nayo; 26 ukamjengee Bwana, Mungu wako, madhabahu juu ya ngome hii, kwa taratibu zake; ukamtwae yule ng'ombe wa pili na kumtoa awe sadaka ya kuteketezwa, kwa kuni za ile Ashera uliyoikata. 27 Ndipo Gideoni akatwaa watu kumi miongoni mwa watumishi wake, akafanya kama Bwana alivyomwambia; lakini ikawa kwa sababu aliwaogopa watu wa nyumba ya baba yake, na watu wa mji, hakuweza kuyatenda hayo wakati wa mchana, basi aliyatenda usiku. 

28 Hata watu wa mji walipoondoka asubuhi na mapema, tazama, madhabahu ya Baali imebomolewa, na ile Ashera iliyokuwa karibu nayo imekatwa, na yule ng'ombe wa pili ametolewa sadaka juu ya ile madhabahu iliyojengwa. 29 Wakaambiana, Ni nani aliyetenda jambo hili? Hata walipotafuta habari na kuuliza, wakasema, Gideoni, mwana wa Yoashi, ndiye aliyetenda jambo hili. 30 Ndipo watu wa mji wakamwambia Yoashi Mlete mwanao, afe; kwa sababu ameibomoa madhabahu ya Baali na kwa sababu ameikata ile Ashera iliyokuwa karibu nayo. 31 Yoashi akawaambia watu wote waliokuwa wakishindana naye, Je! Mtamtetea Baali? Au mtamwokoa ninyi? Yeye atakayemtetea na auawe hivi asubuhi; kama yeye ni Mungu, na ajitetee nafsi yake, kwa sababu mtu mmoja ameibomoa madhabahu yake. 32 Basi akamwita Yerubaali siku hiyo, akisema, Baali na atete naye kwa ajili ya nafsi yake, kwa sababu ameibomoa madhabahu yake.

Somo letu kwa kiasi kikubwa liko ndani haya maandiko, kwaiyo soma kwa kurudia rudia hii habari kabla ya kuendelea, maana ukipata picha ya hapa itakusaidia saana tunakoelekea. Haleluya haleluya !!!

Tunapotafakari kwa kuangalia mambo kadhaa juu ya hali ya ndugu huyu kulingana na maandiko, nawe pia jipime au jitazame kama uko ndani ya hali au mazingira ya namna hii au laah!! Weka picha ya maisha ya Gidioni katika mazingira ya uhalisia kwamba haya mambo yapo kwa kutazama wewe binafsi, familia, majirani, jamaa na jamii ulipokuwa na ulipo kwa sasa ili upate msukumo ndani yako wa kuona sababu ya kushughurikia madhabahu au sababu, kiu na hamu ya kutaka kujitoa katika madhabahu za giza kadri ya utakachopata.
Mambo ya kutafakari  


01.  Kazi aliyokuwa anaifanya Gidioni.
Waamuzi 6:11, Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani.
Kulingana na maandiko yanavyoeleza kijana Gideoni alikuwa pale mwaloni akipepeta ngano ndani ya shinikizo. Maana yake, kazi yake ilikuwa ni ya kupepeta ngano. Tunaelewana mpaka hapo ?? Lakini pia eneo, sehemu au mahali alipokuwa anafanyia kazi hapakuwa eneo lake yaani pale mwaloni, mwaloni uliokuwa Ofra ulikuwa mali ya baba yake mzee Yoashi. Maandiko hayaweki wazi kama alikuwa anapepeta ngano yake binafsi au ya baba yake yaani familia.

Mungu alipomuumba Gideoni kuna kiwango cha hali ya maisha alichokikusudia akiishi cha kumtukuza Mungu ambacho hicho kiwango kinaambatana na aina ya kazi ya kufanya inayoendana na hali ya maisha yake katika mifumo yote ya maisha, mfano- uchumi wa mtu binafsi.
Kazi aliyokuwa akiifanya Gideoni ilikuwa kama kazi isiyokuwa na thamani, heshima, isiyokuwa na kipato, kazi ya kudharauliwa, kazi za watu masikini au kazi za vijana wa hali ya chini kiuchumi. Sasa fikiri kazi za namna hii na maisha yako binafsi, familia, kundi rika au jamii na piga picha kazi uliyonayo. Pia jiulize wewe kazi yako ni ipi?
Mungu alipotaka kumtoa katika hali ya maisha ya namna hii alimpa jukumu la kufanya ili hali ya maisha yake yabadirike. Gideoni aliambiwa kubomoa madhabahu aliyokuwa nayo baba yake? Kwanini abomoe madhabahu ya baali ya baba yake? Kwa sababu madhabahu ya baba yake kama mkuu wa familia ilikuwa inatengeneza hali ya maisha ya wana familia wote akiwemo Gideoni, ivo kama Gideoni akitaka kutoka katika hali ya namna hiyo ilimlazimu kuvunja, kubomoa na kuharibu madhabahu inayohusika na kiwango cha hali ya maisha yake.  
02.  Umasikini wa familia nzima.

Waamuzi 6:15, Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu. 
Mazungumzo ya Mungu na Gideoni yalivyokuwa yanaendelea, Gideoni alikuwa anajaribu kuelezea hali halisi ya maisha yake binafsi pamoja na familia yake. Anasema hivi; jamaa zangu ndio masikini sana katika kabila ya Manase. Maana yake kabila la Manase lilikuwa na familia au kaya tofauti tofauti zenye hali tofauti kimaisha hasa kiuchumi, na kaya ya ndugu za Gideoni ilikuwa masikini saana katika eneo hilo.
Alipojibu kuwa ndugu zangu ndio masikini saana, alimaanisha kuwa ndani ya familia yao wote ni masikini hakuna cha dada wala kaka, mkubwa wala mdogo woote ni masikini. Kwakuwa ni masikini saana basi hata hakuna atakaye msaidia kifedha katika masuala ya huduma na utumishi.
Kwa jinsi ya sasa ni aina ya umasikini ambao; unashinda shule lakini katika ndugu wote hakuna wa kukusaidia, mmojawapo akiumwa ndugu wote wanasukumana tu na mgonjwa anaweza akapoteza maisha kisa ndugu wote hawana kitu, ukipatwa na kesi ghafla unakosa hata wa kukuthamini na unafugwa kwa sababu ya kukosa pesa tu ambayo ni ya kawaida kabisa, familia nyingine ukizitazama ni kama vile hakuna mkubwa na mdogo, ndugu wote wameishia darasa la saba, hawakusoma shule au hawakuimaliza na hawana pa kushikilia n.k

Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, maana yake familia yake ni familia ambayo haina sauti pale kijijini, mjini, kanisani n.k. Au ni familia ambayo haina nafasi, haisikilizwi, inadharauliwa. Sasa kwa kujua ivo akilini mwake alijua kabisa kuwa hata kama Mungu akimtuma bado yeye hatasikilizwa na jamii kwasababu wanaweza wakamdharau kwa sababu ya umasikini wake. Bado hii sio sababu hata kwako leo!!!
Sasa sikia, kilichotengeneza familia nzima kuwa masikini tena sana ni kitu gani? Maisha ya hapa duniani yanaamuriwa kwa kiasi kikubwa na madhabahu tunazozitumikia ivo madhabahu ya mzee Yoashi ilihusika na hali ya maisha yake binafsi pamoja na familia yake yaani hali ya maisha ya watoto wake. Na Mungu alipotaka kumtoa katika hali ya umasikini uliokithiri namna hiyo alimwambia madhabahu. Unasikia ninachosema?? Nasema madhabahu zinatengeneza hali ya maisha kwa watu walio chini ya hiyo madhabahu husika.

03.  Kujidharau kiumri kwa ngazi ya familia kulingana na mira na desturi za jamii.
Waaamuzi 6: 15, Akamwambia, Ee Bwana, nitawaokoa Israeli kwa jinsi gani? Tazama, jamaa zangu ndio walio maskini sana katika Manase, na mimi ndimi niliye mdogo katika nyumba ya baba yangu.
Gideoni anamjibu Mungu kuwa, katika ndugu zangu wote mimi ndiye mdogo katika nyumba ya baba yangu. Akijaribu kumaanisha kuwa kulingana na mira na desturi za familia yetu, ukoo au kabila kuna baadhi ya kanuni, taratibu, sheria, mienendo na miiko ambayo tunaifuata na mojawapo ni mtu aliye mdogo kutofanya jambo fulani ambalo wakubwa zake bado hawalifanya na kwasababu hiyo eeh Bwana nakuomba hii kazi ukawape wakubwa wangu.
Mwanzo 29:25-26, Ikawa, kulipokuwa asubuhi, kumbe! Ni Lea. Akamwambia Labani, Nini hii uliyonitenda? Sikukutumikia kwa Raheli? Mbona umenidanganya? Labani akasema, Havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa;

Unaona kitu alichofanyiwa Labani hapa kulingana na tamaduni za jamii ile? Yeye alifanya kazi miaka saba kwa mzee Labani ili baada ya mda huo apewe binti aliyekuwa amempenda kwa uzuri wake lakini baada ya miaka yooote saba hakupewa huyo binti mdogo mzuri bali alipewa dada yake aliyeitwa Lea. Na Yakobo alipouliza kwanini amefanyiwa mchezo wa namna hiyo, aliambwa hivi; havitendeki hivi kwetu, kumtoa mdogo kabla ya mkubwa. Kwa maana nyingine kulingana na tamaduni zao inabidi kuolewa au kuoa aliye mkubwa kwanza kabla ya mdogo. Vipi wewe kwenyefamilia au jamii kuna mira za namna hii? Jiulize ni wewe hapo umemaliza miaka saba alafu unaambiwa kijana umechemka aisee! Kisa ni tamaduni.

Nadharia ya namna hii ilimfanya hata Gideoni alipotokewa na malaika kutaka kukataa wito wake ambao ndo utakaobadirisha maisha ya baadae kwa sababu ya umri. Kumbuka hii ilikuwa ni fursa ya kubadirisha maisha yake kwa msaada wa Mungu aliyehai.

Mazingira ya namna hii yalitengenezwa na wakuu wa eneo, wazee, washauri au wazee wa busara wa eneo hilo ambapo baadhi yao au miongoni mwao walikuwa wanatumikia madhabahu za giza kama mzee Yoashi, ivo hofu au utii wa tamaduni za namna hii haukuwa kwa jinsi ya mfumo wa Mungu aliyehai bali chimbuko lake lilikuwa ni madahabahu za giza. Ndo maana Mungu alimwagiza Gideoni kuondoa kwanza kinachoachilia roho za kujidharau, kujiona huwezi kulingana na mira na desturi zenye kulenga kukubana ndani yake. Bwna Yesu asifiwe!! Haleluya haleluya.

1Samweli 16:6-13,  Ikawa walipokuja, alimtazama Eliabu, akasema, Yakini masihi wa BWANA yupo hapa mbele zake. Lakini Bwana akamwambia Samweli, Usimtazame uso wake, wala urefu wa kimo chake; kwa maana mimi nimemkataa. Bwana haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali Bwana huutazama moyo. Ndipo Yese akamwita Abinadabu, akampitisha mbele ya Samweli. Naye akasema, Bwana hakumchagua huyu. Ndipo Yese akampitisha Shama. Naye akasema, wala Bwana hakumchagua huyu. Yese akawapitisha wanawe saba mbele ya Samweli. Samweli akamwambia Yese, Bwana hakuwachagua hawa. Kisha Samweli akamwambia Yese, Watoto wako wote wapo hapa? Naye akasema, Amesalia mdogo wao, na tazama, anawachunga kondoo. Basi Samweli akamwambia Yese, Tuma watu, wamlete; kwa sababu hatutaketi hata atakapokuja huku. Basi akatuma mtu, naye akamleta kwao. Naye alikuwa mwekundu, mwenye macho mazuri, na umbo lake lilikuwa la kupendeza. Bwana akasema, Ondoka, umtie mafuta; maana huyu ndiye. Ndipo Samweli akaitwaa pembe yenye mafuta, akamtia mafuta kati ya ndugu zake; na roho ya Bwana ikamjilia Daudi kwa nguvu tangu siku ile. Basi Samweli akaondoka, akaenda zake Rama.

Hapa unaona jambo lililotaka kutokea kwa Daudi, Mungu alimchukulia Daudi tofauti na wengine walivyomchukulia kwa sababu za kwao wenyewe za kibinadamu. Kuanzia kwa baba yake pamoja na mtumishi mwanzoni alipofika ndani ya nyumba ya mzee Yese. Hawakutambua mapema kitu kilichokuwa juu ya Daudi kwa ajili ya Bwana, nah ii ilisababisha huyo motto, kuishi katika mazingira aliyokuwemo mpaka mkono wa Bwana ulipodhihirishwa juu yake, na mkono wa Mungu ulikuwa tofauti na mazingira aliyokuwa akiishi pamoja na nje ya akili za baba yake pamoja na mtu wa Mungu. Hata wewe Mungu anakutazama tofauti na mira, desturi au mazingira uliyomo.

Kwaiyo maisha ya kifamilia au ndoa ya binti Lea kidogo yakwamishwe na mira na tamaduni za ukoo wao, maisha ya Daudi ya utumishi na ufalme yaani kulitumikia kusudi la Mungu kidogo pia yakwamishwe na mtumishi, ndugu akiwemo baba yake pamoja na mazingira, maisha ya Gideoni kidogo yalikwamishwa na baba yake pamoja na mazingira. Mira na desturi au tamaduni za kifamilia, ukoo, kabila au eneo na jamii ilitaka kukwamisha maisha ya hawa ndugu ya hapa duniani. Lakini Mungu wetu azuiliwi na mambo ya tamnaduni, kwaiyo nawe haijalishi unazuiwa na jambo gani la kiutamaduni lenye muunganiko wa kimadhabahu, bado Kristo yupo kwa ajili yako.

04.  Thamani ya Gideoni.
Waamuzi 6:11-12, Malaika wa Bwana akaenda akaketi chini ya mwaloni uliokuwa katika Ofra, uliokuwa mali yake Yoashi, Mwabiezeri; na mwanawe Gideoni alikuwa akipepeta ngano ndani ya shinikizo, ili kuificha machoni pa Wamidiani. Malaika wa Bwana akamtokea, akamwambia, Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa
Hapa tunaona thamani ya Gideoni katika mazingira mawili tofauti, maisha yake ya mwilini hapa duniani na maisha yake ya kiroho yaani mbinguni.
v  Thamani ya Gideoni hapa duniani. Thamani yake hapa duniani ulikuwa ya chini saana kwasababu ya umasikini wake pamoja na familia yake kwa ujumla. Hii ilimsababisha yeye kujiusisha na shughuri za kudharauliwa, kazi zenye pato dogo au zenye faida ndogo. Maisha yake ya hapa duniani yalikuwa ya taabu saana, shida, mihangaiko nay a nguvu saaana kiasi yeye binafsi kujiona si kitu katika maisha haya kwa familia, ndugu, kabila na jamii pia. Maana ni kama vile alikuwa na thamani ndogo mno kiasi kwamba ni kama vile hana thamani yoyote hapa duniani. Unajua mbinguni walimwonaje?

v  Thamani ya Gideoni kule mbinguni. Mbinguni walipomtazama Gideoni walimwonaje? Malaika wa Mungu, wenye uhai wanne, wazee 24, watakatifu na Mungu mwenyewe alimwona Gideoni mtu mmoja mkubwa mno kule mbinguni, mwenye mafanikio, mshindi, mwenye maisha ya hali ya juu saana, mtumishi mmoja mkubwa mno, mtu aliyefanikiwa. Thamani aliyokuwa nayo GIdeobi kule mbinguni ilisababisha serikali ya mbinguni kutuma mwakilishi wao yaani malaika wa kuja kumwambia kuwa; Bwana yu pamoja nawe, Ee shujaa. Unasikia ewe shujaa? Unajiuliza nani shujaa hapa kwa kushanga !!!! ni wewe shujaa wa leo uliyembeba Kristo ndani yako. Bwna Yesu asifiwe! Bwana Yesu asifiwe!

Kwaiyo Gideoni alikuwa na thamani mbili tofauti. Maisha aliyopangiwa kuishi tangu kuumbwa kwake toka mbinguni ni tofauti saana na maisha aliyokuwa akiishi hapa duniani. Na hakujua kuwa yeye mbinguni anaitwa shujaa mpaka neema ya Mungu ilpokuwa juu yake, alijishangaa kuona mbinguni wanamwita yeye kuwa ni shujaa. Inawezekana nawe unaishi maisha kama ya Gideoni tena na kuzidi lakini maadamu umeokoka na kumpokea Kristo Yesu sikia neno hili, wewe ni mtu mkubwa saana na una thamani kubwa mno na ushujaa ulio juu yako ni zaidi ya ule wa Gideoni maana we uko ndani ya agano jipya. unasema sasa mbona niko naishi maisha ya namna hi indo maana unajifunza somo hili ili ukajinasue katika hali yako na ukawe huru kwa jina la Yesu. Haleluya Haleluya

Mariko 11:1-10, Hata walipokaribia Yerusalemu karibu na Bethfage na Bethania, kukabili mlima wa Mizeituni, aliwatuma wawili katika wanafunzi wake, akawaambia, Nendeni mpaka kile kijiji kinachowakabili; na katika kuingia ndani yake, mara mtaona mwana-punda amefungwa, asiyepandwa na mtu bado; mfungueni, kamleteni. Na mtu akiwaambia, Mbona mnafanya hivi? Semeni, Bwana anamhitaji na mara atamrudisha tena hapa. Wakaenda zao, wakamwona mwana-punda amefungwa penye mlango, nje katika njia kuu, wakamfungua. Baadhi ya watu waliosimama huko wakawaambia, Mnafanya nini kumfungua mwana-punda? Wakawaambia kama Yesu alivyowaagiza, nao wakawaruhusu. Wakamletea Yesu yule mwana-punda, wakatandika mavazi yao juu yake; akaketi juu yake. Watu wengi wakatandaza mavazi yao njiani, na wengine matawi waliyoyakata mashambani. Nao watu waliotangulia na wale waliofuata wakapaza sauti, Hosana; ndiye mbarikiwa ajaye kwa jina la Bwana; umebarikiwa na ufalme ujao, wa baba yetu Daudi. Hosana juu mbinguni.

Ukisoma haya maandiko ndani yake kuna vitu vya ajabu mno, unaona thamani ya mwana-punda katika mazingira mawili tofauti. Licha kuwa ndani ya haya maandiko kuna unabii wa kipekee aliokuwa akiusema Yesu, lakini tuangalaie hasa juu ya thamani ya mwana- punda. Tunaona punda akiwa na thamani mbili tofauti; moja ni katika hali ya kufungwa akiwa amefungwa kule ndani kijijini na thamani yake ya pili ni ile aliyoipata alipokuwa na Yesu au alipopandwa na Yesu. Hizi ni thamani mbili tofauti kabisa, uanelewa jambo nasema hapa? Kuwa thamani yako kabla ya kumpokea Yesu na baada ya kumpokea umekuwa na thamani ambayo haukuwa nayo kabisa.

Kuna watu ambao hawakutaka yule mwana- punda afunguliwe ndo maana waliwauliza wale waliokuwa wanamfungua waliokuwa wametumwa na Bwana Yesu, kuwa “Mnafanya nini kumfungua mwana-punda?” sijui walikuwa na faida gani katika kufungwa kwa huyo punda lakini au ni kwa kwanini walitaka yule mwana punda abakie katika maisha yaleyale ya kufungwa. Kwa maana nyingine hawakutaka punda apate heshima akiwa pamoja na Yesu, hawakutaka punda atoke katika hali aliyokuwa nayo. Mungu mwenyewe alipooona vema juu ya aliyemchagua alimtokea kuja kumfungua toka katika hali ya aliyokuwa nayo na mahali alipokuwa. Sasa unaona picha ya thamani ya Gideoni mbele za Bwana ilivyokuwa tofauti na mazingira pamoja na jamii hasa wale waliokuja wakitaka kumwua Gideoni kama wale waliouliza kwanini mnamfungua huyo mwana-punda?

Tutaendelea na somo hili kadri ya neema ya Mungu na msukumo, nikukaribishe ndugu katika Kristo kwa ajili ya kufuatilia somo hili linalohusiana na masuala ya Madhabahu. 




2 comments: